Swali: Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ametukataza kuanza kuwatolea makafiri Salaam. Je, makatazo haya yanaishia kuwaambia “as-Salaam ´alaykum wa Rahmatullaah” au ni makatazo ambayo kunaingia ndani yake mamkizi aina yote? Je, inajuzu kuanza kumsalimia jirani ambaye ni mnaswara kinyume na kusema “as-Salaam ´alaykum wa Rahmatullaah” kama kumwambia “Khabari yako”, “Vipi hali yako” au “Khabari ya asubuhi”?
Jibu: Haijuzu kuanza kumtolea kafiri Salaam kutokana na yaliyothibiti kutoka katika Hadiyth ya Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye ameeleza kuwa Mtume wa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Msianze kuwatolea mayahudi na manaswara Salaam, mkikutana na mmoja wao njiani basi mbane kandoni.”
Ameipokea Muslim.
Anas (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ahl-ul-Kitaab wakikusalimieni waambieni “wa ´alaykum.”
Wanatakiwa kuitikiwa kutokana na udhahiri wa Hadiyth kwa kuambiwa:
“wa ´alaykum.”
Hata hivyo hakuna ubaya kumsalimia kafiri kwa kumwambia:
“Vipi hali yako”, “Umeamkaje”, “Umelalaje” na mfano wa maamkizi kama hayo kukiwa kuna haja ya kufanya hivo. Hivyo ndivyo wanavyoonelea baadhi ya wanachuoni ikiwa ni pamoja na Abul-´Abbaas Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah).
- Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (3/312)
- Imechapishwa: 23/08/2020
Swali: Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ametukataza kuanza kuwatolea makafiri Salaam. Je, makatazo haya yanaishia kuwaambia “as-Salaam ´alaykum wa Rahmatullaah” au ni makatazo ambayo kunaingia ndani yake mamkizi aina yote? Je, inajuzu kuanza kumsalimia jirani ambaye ni mnaswara kinyume na kusema “as-Salaam ´alaykum wa Rahmatullaah” kama kumwambia “Khabari yako”, “Vipi hali yako” au “Khabari ya asubuhi”?
Jibu: Haijuzu kuanza kumtolea kafiri Salaam kutokana na yaliyothibiti kutoka katika Hadiyth ya Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye ameeleza kuwa Mtume wa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Msianze kuwatolea mayahudi na manaswara Salaam, mkikutana na mmoja wao njiani basi mbane kandoni.”
Ameipokea Muslim.
Anas (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ahl-ul-Kitaab wakikusalimieni waambieni “wa ´alaykum.”
Wanatakiwa kuitikiwa kutokana na udhahiri wa Hadiyth kwa kuambiwa:
“wa ´alaykum.”
Hata hivyo hakuna ubaya kumsalimia kafiri kwa kumwambia:
“Vipi hali yako”, “Umeamkaje”, “Umelalaje” na mfano wa maamkizi kama hayo kukiwa kuna haja ya kufanya hivo. Hivyo ndivyo wanavyoonelea baadhi ya wanachuoni ikiwa ni pamoja na Abul-´Abbaas Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah).
Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (3/312)
Imechapishwa: 23/08/2020
https://firqatunnajia.com/muislamu-kuanza-kumsalimia-kafiri/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)