Swali: Muda mwingi wa mlinganizi unatakiwa kuwekwa katika kujifunza elimu?
Jibu: Kutegemea na wepesi wake:
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
”Basi mcheni Allaah muwezavyo.”[1]
Mlinganizi anaweza kuwa na haja ambayo hakuna wa kumtekelezea nayo. Vilevile pengine akawa na haja ili kuweza kuwahudumia familia yake. Kwa hivyo atenge wakati wa kujifunza elimu, kulingania na kutoa miongozo na wakati mwingine kwa ajili ya kutafuta riziki. Kutafuta riziki hakumzuii mtu kulingania kwa muuzaji, mnunuzi, mmiliki wa duka, anayempitia, anayesimama pamoja naye na kadhalika. Kujifunza elimu ni jambo jepesi kila mahali.
[1] 64:16
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22964/هل-يكون-جل-وقت-الداعية-للعلم
- Imechapishwa: 22/09/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)