Swali: Muadhini akisema wakati wa kuadhini:

أشهدُ أنَّ محمَّدًا عبد الله ورَسولُه

”Nashuhudia ya kwamba Muhammad ni mja wa Allaah na Mtume Wake.”

badala ya:

أَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّداً رَسُولُ الله

”Nashuhudia ya kwamba Muhammad ni Mtume wa Allaah.”

Je, analazimika kuirudia sentesi hii?

Jibu: Ndio. Adhaana haibadilishwi, haizidishwi na wala haipunguzwi. Inatakiwa kusomwa kama ilivyopokelewa.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (40)
  • Imechapishwa: 19/05/2023