Swali: Ni vipi kutofautisha kati ya machukizo kwa njia ya mapendezo na machukizo kwa njia ya uharamu?
Jibu: Msingi katika makatazo ni uharamu. Huu ndio msingi. Isipokuwa yale yanayofahamishwa na dalili. Ni kana kwamba wamechukua jambo hilo katika njia ya adabu na du´aa na si katika mambo ya wajibu. Ni kana kwamba wamechukua hilo katika maana. Msingi katika maamrisho ni uwajibu. Msingi katika makatazo ni uharamu. Huu ndio msingi.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23020/ما-الفرق-بين-كراهة-التنزيه-وكراهة-التحريم
- Imechapishwa: 13/10/2023