Swali: Tuna ndugu ambao wanamtukana Allaah (Jalla wa ´Alaa) na dini. Je, tuwatembelee wanapogonjweka au tuwakate?

Jibu: Ikiwa wanakubali Da´wah na inawaathiri watembeleeni. Walinganie katika dini ya Allaah na tawbah. Wabainishieni haki na wakatazeni na hicho walichoshikamana nacho. Huenda Allaah akawaongoza. Ama ikiwa hawakubali haki na wanaipuuza, jitengeni nao mbali:

إِنَّكَ لَا تَهْدِي مَنْ أَحْبَبْتَ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَهْدِي مَن يَشَاءُ ۚوَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ

“Hakika wewe huwezi kumwongoza umpendaye, lakini Allaah humowngoza amtakaye – Naye anawajua zaidi waongokao.” (28:56)

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Tafsiyr-ish-Shaykh Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (22) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tafsirayat-05-07-1435-01.mp3
  • Imechapishwa: 19/06/2020