Swali: Wakati fulani mtu anapita karibu na mnaswara au myahudi au ambaye hajui hali yake. Je, ampe salamu?
Jibu: Amsalimie yule atayekutana naye. Kama ambavo amesema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) baada ya kuulizwa: “Ni Uislamu ipi bora?” Akasema:
“Kulisha chakula na kumtolea salamu unayemjua na usiyemjua.”
Isipokuwa ukijua kuwa ni myahudi, mnaswara au makafiri wengine basi usianze kuwasalimia. Lakini usipojua msalimie utayekutana naye.
Swali: Vipi akiwa na haja kwake?
Jibu: Asimtolee salamu. Amuulize hali yake, anavyoendelea na hali ya watoto wake. Asimwambie:
السلام عليكم
“Amani ya Allaah iwe juu yenu.”
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23465/حكم-القاء-السلام-على-من-لا-يعلم-بحالهم
- Imechapishwa: 26/01/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket