Mke kumueleza mume wake sifa za wanawake wengine

Swali: Mume wangu anataka nimueleze sifa za baadhi ya wanawake. Je, nikifanya hivyo itakuwa tendo hili ni katika maasi?

Jibu: Ikiwa anataka kumposa mwanamke huyu ndio maana anataka umueleze sifa zake, hakuna neno. Ama ikiwa anataka kupeleleza wanawake na kujua mazuri ya wanawake, hili ni jambo lisilojuzu. Ukimtii utakuwa umesaidiana nae katika maasi na uadui.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/ls–1428-03-04.mp3
  • Imechapishwa: 22/09/2020