Swali: Je, inafaa kwa mwanamke aliye ndani ya eda ya kufiwa na mume wake kutoka kwenda kufanya ´Umrah?
Jibu: Hapana. Asitoke kwa ajili ya kufanya ´Umrah wala Hajj mpaka imalizike eda. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema kuhusu mwanamke aliyefiwa na mume wake:
“Baki nyumbani mpaka eda imalizike.”
Lakini ikiwa mume atakufa ilihali mwanamke huyu yuko njiani? Wamesema ikiwa ameshafika ule umbali unaoruhusu kufupisha swalah, basi ataendelea katika ´Umrah au Hajj yake. Ikiwa ni chini na yale masafa yanayoruhusu kufupisha, basi anatakiwa kurejea katika nyumba yake.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/eg–14041434.mp3
- Imechapishwa: 10/04/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)