Imaam an-Nawawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
وعن أنس ـ رضي الله عنه ـ قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((إذا أراد الله بعبده خيرا عجل له العقوبة في الدنيا، وإذا أراد بعبده الشر أمسك عنه بذنبه حتى يوافي به يوم القيامة))
43 – Anas (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah anapompendelea mja wake kheri, basi humharakishia adhabu duniani, na akimtakia mja wake shari humzuilia dhambi zake ili amuadhibiwa kwazo siku ya Qiyaamah.”
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika malipo makubwa yanakuwa pamoja na mabalaa makubwa. Allaah (Ta´ala) anapowapenda watu, huwapa majaribio; yule anayeridhia basi hupata radhi [za Allaah], na yule mwenye kuchukia hupata khasira [za Allaah].”
Hadiyth ni nzuri
Matatizo mepesi yana malipo madogo. Matatizo mazito yana malipo makubwa. Allaah ni mwingi wa fadhilah kwa watu. Akiwapa mtihani kwa matatizo makubwa, basi anawalipa kwa ujira ulio mkubwa. Matatizo mepesi yana ujira mdogo.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Riyaadh-is-Swaalihiyn (01/259)
- Imechapishwa: 12/03/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)