Swali: Nilimkataza mke wangu vazi ambalo wanachuoni walitoa Fatwa kutojuzu kulivaa kwa kumwambia “wewe kwangu ni haramu [ukivaa]”. Mara ya kwanza akaitikia, lakini hata hivyo akalivaa kwa mara ya pili kwa kusahau – kama alivyosema. Ni lipi la wajibu juu yangu katika hali kama hii?
Jibu: Masuala haya yanahitajia kuzingatiwa. Ni jambo lenye julikana ya kwamba watu ni wenye kupewa udhuru [wakati wa kusahau]. Allaah Amesema:
لَا يُكَلِّفُ اللَّـهُ نَفْسًا إِلَّا وُسْعَهَا |
”Allaah Hakalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya uwezo wake.” (02:286) |
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Ummah wangu ni wenye kusamehewa makosa ya kusahau na waliyotenzwa nguvu.”
Masuala haya yanatakiwa kuzingatiwa. Ninachomnasihi muulizaji aende [katika baraza] la kufutu.
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajhiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://subulsalam.com/play.php?catsmktba=11647
- Imechapishwa: 01/05/2015
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)