Swali: Je, Sutrah ni lazima?
Jibu: Ni Sunnah iliyokokotezwa kwa anayeswali peke yake na imamu.
Swali: Wale watu aina tatu wanaoharibu swalah wanapopita mbele ya mswaliji[1] mtu anatakiwa kuanza upya?
Jibu: Ndio, mtu huyo akipita karibu na mswaliji au akapita baina ya mswaliji na Sutrah. Linamuhusu imamu na anayeswali peke yake. Kuhusu maamuma haiwadhuru. Mpitaji akipita mbele ya maamuma haiwadhuru kitu.
Swali: Imethibiti kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliswali pasi na Sutrah?
Jibu: Ndio.
Swali: Kwa hivyo katika hali hiyo ina maana kwamba mtu wakati mwingine aswali pasi na Sutrah?
Jibu: Ndio. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakati mwingine aliswali pasi na Sutrah.
Swali: Kwa hivyo mtu anaweza pia kuswali bila ya Sutrah?
Jibu: Pale ambapo atashindwa kupata Sutrah, ingawa bora ni kuswali mbele ya Sutrah.
[1] Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Swalah ya mtu muislamu inakatika kusipokuwa mbele yake mfano wa bakora ya anayepanda kipando: mwanamke, punda na mbwa mweusi.” (Muslim)
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23015/حكم-السترة-للمصلي-وحكم-من-قطعت-صلاته
- Imechapishwa: 15/10/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)