Swali: Vipi kuhusu kufunga swawm inayopendeza baada ya nusu Sha´baan?
Jibu: Ikiwa hakuanza kufunga katika ile nusu ya kwanza, basi asifunge nusu iliyobakia.
Swali: Nakusudia swawm ya kujitolea yoyote?
Jibu: Hapana neno akaendelea kufunga jumatatu na alkhamisi. Ikiwa ana mazowea ya kufunga jumatatu na alkhamisi hapana neno.
Swali: Swawm ya masiku meupe?
Jibu: Swawm ya masiku meupe inaanza kabla ya nusu ya kwanza.
Swali: Vipi kwa mfano akiichelewesha?
Jibu: Hapana, swawm ya masiku meupe inakuwa tarehe 13, 14 na 15. Hizi ndio tarehe za swawm ya masiku meupe.
Swali: Akianza kunuia baada ya tarehe 15?
Jibu: Hapana, asianze. Kutokana na Hadiyth:
“Sha´baan inapofika katikati, msifunge.”
Swali: Kama alifunga siku moja katika nusu ya kwanza ya Sha´baan aendelee kufunga nusu ya pili?
Jibu: Udhahiri wake ni kwamba haina neno. Kama alianza kufunga siku kadhaa kabla yake hapana vibaya akaendelea. Muhimu ni yeye afunge siku nyingi za Sha´baan.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22826/ما-حكم-صوم-التطوع-بعد-انتصاف-شعبان
- Imechapishwa: 28/08/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)