Swali: Mwanamke akijiingiza vidole vyake ukeni kwa ajili ya kujisafisha, kuingiza marashi, tembe kwa ajili ya matibabu au baada kugundua maradhi ya wanawake ambapo daktari wa kike ndiye ameingiza mkono wake au kifaa cha ugunduzi – je, mwanamke huyu atalazimika kuoga? Je, mwanamke huyu atafungua ikiwa yamefanyika mchana wa Ramadhaan na hivyo atalazimika kulipa?

Jibu: Yakitokea haya yaliyotajwa hatolazimika kuoga josho la janaba na wala haitoharibika funga yake.

´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz

´Abdur-Razzaaq ´Afiyfiy

´Abdullaah bin Ghudayyaan

  • Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (10/174) nr. (9881)
  • Imechapishwa: 28/04/2022