Mama ananiomba pesa ili awape wadogo zangu wasotaka kufanya kazi

Swali: Kuna mtu anaombwa pesa na mama yake ili awape watoto wake wakubwa na hilo linawafanya kukosa ajira na kufanya kazi. Je, akimuomba pesa kwa lengo hili ampe?

Jibu: Ikiwa anchukua mali kutoka kwako na kuwapa ndugu zako hili halijuzu kwake yeye. Ama kuhusu wewe mpe ili uweze kumridhisha. Kuhusu ya kwamba anazitumia kwa njia ya kinyume yeye ndiye ataulizwa juu ya hilo. Lakini hata hivyo yeye asimnyime pesa maadamu ana uwezo wa kufanya hivo.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/al_makruf%203-12-08-1433.mp3
  • Imechapishwa: 16/06/2015