Mali ya mke anayomuazima mume wake

Swali: Nilimnunulia mke wangu dhahabu. Wakati nilipohitajia kiwango cha pesa akaniuzia kwa ridhaa yake na nikatumia mali hiyo. Je, ni lazima kwangu kumrudishia wakati atakaponiomba hilo?

Jibu: Ikiwa ameikupa na akakuruhusu [kuitumia], sio wajibu kumrudishia. Ama ikiwa ameikupa kwa sharti umrudishie nayo [baadaye] au umrudishie kiwango badala yake, ni wajibu kumrudishie. Isipokuwa tu ikiwa kama atakusamehe.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/montqa14340202.mp3
  • Imechapishwa: 19/09/2020