Swali: Kukaribiana masoko ni katika alama za Qiyaamah?
Jibu: Imekuja katika Hadiyth Swahiyh ya kwamba zama zitakaribiana. Kuhusu masoko ni maneno tu ya watu. Alama za Qiyaamah ni kukaribiana kwa zama, mauaji yatakuwa mengi na pombe zitanywiwa kwa wingi. Yote haya yatakuwa katika zama za mwisho. Ameyaeleza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kama ilivyokuja katika al-Bukhaariy na kwenginepo.
Swali: Ni nini makusudio ya zama kukaribiana?
Jibu: Bi maana mwaka utakuwa kama mwezi, mwezi utakuwa kama wiki na wiki itakuwa kama siku moja. Kwa maana nyingine wakati utaenda haraka sana na baraka itakuwa chache.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22666/هل-تقارب-الاسواق-من-علامات-الساعة
- Imechapishwa: 13/07/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)