Makatazo ya kupandisha sauti juu msikitini

Swali: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Enyi watu! Kila mmoja wenu anamnong´oneza Mola wake. Hivyo wamoja wasisome Qur-aan kwa sauti juu ya wengine.”

Kama kuna wamoja wanaosoma Qur-aan na wengine wanaswali na kati yao kukawa ambaye anasoma kwa sauti ya juu. Je, mtu huyo aambiwe kuwa Kila mmoja wenu anamnong´oneza Mola wake na hivyo ashushe sauti yake?

Jibu: Ndio, ambainishie ashushe sauti yake. Kama ambavo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alivyowabainishia wale wanaoswali msikitini:

“Enyi watu! Kila mmoja wenu anamnong´oneza Mola wake. Hivyo wamoja wasisome Qur-aan kwa sauti juu ya wengine.”

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23443/معنى-كلكم-يناجي-ربه-في-الحديث
  • Imechapishwa: 23/01/2024