Maimamu wanaorefusha na kujikakama katika Qunuut

Swali: Baadhi ya maimamu katika Qunuut wanarefusha na wanajikakama. Ni zipi nasaha zako juu ya hilo?

Jibu: Bora ni kufupisha na kutorefusha. Bora ni kutorefusha na kutowatia watu uzito. Aombe du´aa zilizokusanya na asirefushe na wala asiwatie watu uzito. Kufanya hivo ndio bora. Anayewaongoza watu basi akhafifishe. Kwani katika wao kuna mdogo, mtumzima na mnyonge. Hivi ndivo alivosema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/audios/794/فتاوى-رمضانية
  • Imechapishwa: 01/04/2023