Ni wajibu kwa mzinifu apigwe bakora mia na afukuzwe kwenye mji kwa muda wa mwaka. Hili linahusu yule ambaye hajaoa/hajaolewa hapo kabla. Ama ikiwa alioa na kumwingilia mke wake, huyu anapigwa mawe mpaka afe. Yote haya ni ili kuwatisha watu wasitumbukie katika uchafu huu. Uchafu huu unaharibu tabia, dini na ukoo. Ukiongezea juu ya hayo ni kwamba uchafu huu unaleta maradhi makubwa ambayo athari yake imeonekana leo ambapo uchafu wa zinaa umekithiri.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Riyaadh-is-Swaalihiyn (01/306)
  • Imechapishwa: 04/05/2023