Machukizo ya kufunika mapazia ukutani

Swali: Mapazia yasiyokuwa na haja yanayowekwa kwenye madirisha?

Jibu: Hapana vibaya kwenye madirisha. Hata hivyo hapana kwenye kuta. Kama alivosema:

“Ni tangu lini mmekuwa na Ka´bah?”

Lakini ikiwa mapazia yamewekwa madirishani ni sawa kama ambavo kunawekwa milangoni.

Swali: Pindi ´Aaishah alipoweka pazia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikaripia picha na hakukemea pazia yenyewe?

Jibu: Liliwekwa mlangoni. Haina neno kuweka pazia mlangoni na madirishani.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23866/حكم-الستاىر-على-الجدران-والنوافذ
  • Imechapishwa: 23/05/2024