Swali: Je, ni jambo limewekwa katika Shari´ah wakati wa kuomba du´aa?
Jibu: Miongoni mwa sababu za kuitikiwa du´aa ni kunyanyua mikono wakati wa kuomba du´aa. Ni mamoja wakati anaomba katika Qunuut au maeneo mengine. Isipokuwa yale maeneo ambayo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakunyanyua mikono ndani yake. Miongoni mwa maeneo hayo ni baada ya kumaliza swalah ya faradhi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakunyanyua mkono maeneo hayo. Sehemu nyingine ni kati ya sijda mbili wala mwishoni mwa swalah. Akiomba du´aa kabla ya kumaliza swalah asinyanyue mikono kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakunyanyua mikono. Mtu asinyanyua mikono katika maeneo haya ambayo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakunyanyua. Maeneo mengine ni katika Khutbah ya ijumaa na Khutbah ya ´iyd. Isipokuwa tu wakati ambapo imamu ataomba du´aa ya kunyesha mvua hapo ndipo inafaa kwake kunyanyua mikono.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22579/متى-يشرع-رفع-اليدين-في-الدعاء
- Imechapishwa: 06/07/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)