Swali: Baadhi ya watu wanamkopa mtu mkopo akashindwa mkopeshwaji kurudisha wanazingatia mkopo huo kuwa ametoa zakaah.
Jibu: Hapana, deni haliwi zakaah. Ni lazima amsubiri. Atapozishika mkononi atazitoa kama zakaah. Vinginevyo amsaidie kwa pesa isiyokuwa zakaah. Haina neno kama amemwachia nazo kama swadaqah. Kuhusu zakaah haitolewi kutoka kwenye pesa ya deni. Pesa ya zakaah anatakiwa kutoa kile alichonacho. Kuhusu deni amsubiri na ampe muda. Ni mwenye kushukuriwa na mwenye kulipwa thawabu iwapo atamsamehe kwa ajili ya kutafuta radhi za Allaah na asizingatie kuwa ametoa zakaah.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22951/حكم-مدين-يطلب-من-داىنه-اعتبارها-زكاة
- Imechapishwa: 21/09/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)