Swali: Baadhi ya watu wanaweza kumuona mtu yuko na dhambi au nguo iliyovuka kongo mbili za miguu na wasimsalimie.

Jibu: Hapana. Kilichosuniwa ni kutoa salamu na kutoa nasaha. Pengine mtu akawa mjinga. Sunnah ni kutoa salamu, kwa sababu ndani yake kuna faraja na kuwa na ukaribu. Isitoshe jengine ni ufunguo wa kutoa nasaha. Isipokuwa akiwa ni mkaidi na yeye anajua kuwa ni mkaidi na akaona kuwa kumkata ndio kuna manufaa zaidi na kunamuathiri na kumnufaisha zaidi. Akiona kuwa kumkata hakuna manufaa na kwamba kuendelea kumnasihi ndio kunanufaisha zaidi, basi afanye kile chenye manufaa zaidi.

Swali: Anayepita karibu na mvuta sigara amtolee salamu?

Jibu: Ndio, amsalimie na amnasihi. Ambainishie kuwa hayo ni maovu.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23941/هل-يلقى-السلام-على-صاحب-المعصية
  • Imechapishwa: 02/08/2024