Kutoka nje kucheza na kuimba wakati mvua inaponyesha

Swali: Baadhi ya watu kunaponyesha mvua basi wanajitokeza hadharani na wanadhihirisha maasi kama vile nyimbo, kucheza, kuchanganyika na mengineyo. Je, una nasaha zozote za kuwapa watu hawa?

Jibu: Hapana shaka kwamba ni kuzikabili neema kwa maasi. Tunamwomba Allaah usalama. Ni lazima kwao kumshukuru Allaah, walazimiane na kumtii Allaah, watekeleza faradhi za Allaah na wajiepushe na maharamisho ya Allaah. Kudhihirisha maasi ni kuikabili neema kwa kufuru. Tunamwomba Allaah usalama.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (22)
  • Imechapishwa: 30/10/2021