Kutembea au kupanda wakati wa kwenda kuswali ´iyd?

Swali: Je, ni Sunnah kwenda kuswali swalah ya ´iyd kwa kutembea au kwa kupanda?

Jibu: Ni Sunnah kutembea[1]. Lakini kama mtu anahitaji kupanda basi hapana vibaya kupanda.

[1] at-Tirmidhiy (530) aliyesema kuwa ni nzuri. Nzuri kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh Sunan at-Tirmidhiy” (530).

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (16/235)
  • Imechapishwa: 25/04/2026