Swali: Mimi nafanya kazi ya upigaji picha ambazo zinachapishwa katika magazeti au vipeperushi. Ni upi usahihi wa kazi hii?

Jibu: Ikiwa picha hizo zinazo manufaa ya kidini, basi hapana vibaya. Lakini ikiwa hazina manufaa yoyote, basi uchaji na bora zaidi ni kuiacha na kutafuta kazi nyingine, au angalau kwa uchache ujizuilie kuchukua picha vile viumbe vyenye roho.

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/355)
  • Imechapishwa: 25/04/2026