Kusoma Qur-aan na huku mtu anafuatilia kaseti

Swali: Mimi kila asubuhi ninasoma Qur-aan na wakati huohuo kunakuwa na kanda inayosoma Qur-aan. Je, inajuzu kufanya hivo?

Jibu: Ndio, inajuzu kwako kusoma Qur-aan midhali sauti ya kanda haikushughulishi na kusoma na kuzingatia yale unayoyasoma.

  • Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (4/104)
  • Imechapishwa: 22/08/2020