Swali: Kunyoa nywele zote za kichwani katika msimu usiokuwa wa hajj ni katika mwenendo wa Khawaarij?
Jibu: Hapana vibaya akizinyoa na akaona manufaa ya kufanya hivo. Khawaarij wanawalazimisha wafuasi wao kunyoa. Ni katika alama zao. Msingi wa jambo inafaa kwa mujibu wa Shari´ah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alinyoa kipara katika hajj ya kuaga na akapunguza nywele katika ´umrah. Wakati usiokuwa wa hajj na ´umrah inafaa kufanya hivo. Hilo ni kama alivosema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
”Ima nyoa zote au ziache zote.”[1]
[1] al-Muhallaa (7/211).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/21939/حكم-حلق-الراس-كاملا-في-غير-النسك
- Imechapishwa: 03/10/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)