Swali: Ni ipi hukumu ya kung´oa jino? Kuna khatari akameza damu.

Jibu: Katika hali hiyo anameza damu yake mwenyewe. Haliharibu swawm. Hata hivyo ni bora zaidi acheleweshe hilo mpaka wakati ambapo atakuwa hakufunga ili asije kupata madhara wakati amefunga. Vinginevyo ni bora zaidi kuchelewesha hilo mpaka jioni.

  • Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fadhwaaih wa Naswaaih, uk. 80
  • Imechapishwa: 26/08/2020