Swali: Je, ni kweli kuwa unatofautisha kati ya kundi lililonusuriwa na kundi lililookoka?
Jibu: Kundi lililonusuriwa ndio kundi lililookoka. Ni moja.
Swali: Huyatofautishi kati yake?
Jibu: Ni moja.
Swali: X jana jioni alikuwa na muhadhara na akasema kuwa Shaykh ´Abdul-´Aziyz bin Baaz anaafikiana naye juu ya hilo.
Jibu: Hapana, hapana. Kundi lililonusuriwa ndio kundi lililookoka na wao ndio Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah. Wao ni Ahl-us-Sunnah, kundi lililookoka na kundi lililonusuriwa.
Swali: Na wao ni Salafiyyuun?
Jibu: Na wao ni Salafiyyuun. Wao ni kundi lililookoka kwa sababu wameokoka kutokana na Moto, wao ni kundi lililonusuriwa kwa sababu wameahidiwa kunusuriwa na wao ni Ahl-us-Sunnah kwa sababu wanazifuata Hadiyth za Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://www.youtube.com/watch?v=9jJcabonJGM&app=desktop
- Imechapishwa: 21/05/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)