Swali: Je, wanyamahoa waliopotea wanapaswa kutangazwa?
Jibu: Ndiyo, kwa mwaka mmoja. Yeyote anayeokota mnyama aliyepotea, yeye mwenyewe ni mpotevu asipomtangaza. Hili linahusu wanyamahoa tu. Ama ngamia, anapaswa kumwacha, pamoja na ng’ombe, farasi na punda.
Swali: Nini maana ya maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Huyo ni wako, mwenye nao au wa mbwa mwitu.”?
Jibu: Inamaanisha kwamba anapaswa kumtangaza. Usimwache aliwe na mbwa mwitu. Mchukue na mtangaze.
Swali: Je, mtu anapata dhambi ikiwa hakumchukua mnyamahoa kwa sababu ya kuchelea majukumu?
Jibu: Hapana, hapati dhambi. Mnyamahoa huyo ni halali kwake:
”Ni wako, wa ndugu yako au wa mbwa mwitu.”
Lakini kwa sharti la kumtangaza.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/25420/حكم-اخذ-ضالة-الغنم-ومدة-تعريفها
- Imechapishwa: 24/03/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)