Swali: Je, ni lazima kuandika “Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam” wakati anapotajwa katika maandishi?
Jibu: Ndio yenye kudhihiri wakati anapotajwa na wakati unapomsikia. Wakati anapoandikwa na wakati unampomsikia akitajwa. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Hadiyth Swahiyh:
”Liguse mchanga pua la yule ambaye nitatajwa mbele yake na asiniswalie.”
Jibriyl alimwambia:
”Liguse mchanga pua la mja ambaye utatajwa mbele yake na asikuswalie.” Sema: ”Aamiyn.” Nikasema: ”Aamiyn.”[1]
Haya yanajulisha kuwa ni wajibu.
Swali: Vipi ikiwa mtu ataandika “Mtume” kisha akamswalia kwa mdomo na asiandike?
Jibu: Yanafikiwa malengo. Hata hivyo bora aiandike ili amsaidie pia yule msomaji.
[1] Cheni ya wapokezi wake ni nzuri kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Fadhwl-us-Swalaah ´alaan-Nabiy” (18).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23003/حكم-كتابة-الصلاة-والتسليم-لذكر-النبي-ﷺ
- Imechapishwa: 07/10/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)