Swali: Aliyeungua kwa moto anaoshwa?

Jibu: Ikiwezekana. Vinginevyo anafanyiwa Tayammum. Ikiwezekana kumuosha anaoshwa. Ikiwa wanachelea kukatikakatika viungo basi atafanyiwa Tayammum kisha kumswalia. Kama amechomeka kwa moto atafanyiwa Tayammum uso na mikono yake kwa mchanga. Lakini ikiwezekana kumuosha kwa maji kwa njia ya kwamba viungo vyake vimekamatana basi ataoshwa kwa maji.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22931/هل-يغسل-المحروق-بالنار
  • Imechapishwa: 16/09/2023