Swali: Baadhi ya watu wanasema kuwa pombe ina manufaa na kwa ajili hiyo wanainywa. Ni manufaa gani hayo yaliyomo ndani yake?
Jibu: Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
يَسْأَلُونَكَ عَنِ الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ ۖ قُلْ فِيهِمَا إِثْمٌ كَبِيرٌ وَمَنَافِعُ لِلنَّاسِ وَإِثْمُهُمَا أَكْبَرُ مِن نَّفْعِهِمَا
”Wanakuuliza kuhusu pombe na kamari. Sema: “Katika viwili hivyo mna dhambi kubwa na manufaa [fulani] kwa watu; na dhambi yake viwili hivyo ni kubwa kuliko manufaa yake.”[1]
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amemuomba Allaah aondoshe manufaa ya pombe hata kwa lengo la kujitibu. Amesema:
“Allaah asimponye.”
Pombe ni ugonjwa na si dawa. Pombe ina madhara mengi. Kuna faida gani kupoteza akili kwa muda na kisha kuamka ukiwa katika hali mbaya?
[1] 2:219
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 273
- Imechapishwa: 14/04/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)