Swali: Je, inafaa kuingiza video, TV na zana za picha ndani ya msikiti?
Jibu: Hapana, haijuzu. Huku ni kuingiza maovu. Kitendo cha yeye kuwasha redio na ndani yake kukawa kuna kitu katika nyimbo au sauti za madhambi.
Swali: Baadhi ya watu wanajengea hoja ya kufaa kwa kuwepo zana za picha katika msikiti wa Makkah.
Jibu: Hapana, haifai kufanya hivo. Kitendo chao sio hoja. Picha ni haramu kabisa.
Swali: Hata katika msikiti Mtakatifu?
Jibu: Katika msikiti Mtakatifu pia zimekatazwa. Wasimamizi wakichukulia wepesi jambo hilo haijakuwa ni dalili. Kuchukua wepesi mwenye kuchukulia wepesi haiwi hoja.
Swali: Baadhi ya watu wanasema kuhusiana na mashine ulizozitaja punde kidogo kwamba vitu hivyo vinanufaisha ulinganizi na vinawanufaisha watu.
Jibu: Hapana, hapana. Ni sawa ikiwa ni jambo jema peke yake kama vile redio ya Qur-aan. Lakini ndani yake kunaweza kuingizwa matangazo ya vitu visivyokuwa vizuri. Hata hivyo ni sawa ikiwa vitahifadhiwa na mtu akawa anasikia redio ya Qur-aan au vitu vizuri.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22048/حكم-ادخال-الات-التصوير-والفيديو-الى-المسج
- Imechapishwa: 20/10/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)