Swali: Ibn-ul-Qayyim (Rahimahu Allaah) amesema kuwa mwenye kuitafuta dunia kwa lengo la kuwafanyia watu wema basi shaytwaan anakuwa mwenye kumpendezeshea nayo na hivyo anatumbukia katika kuipenda dunia na kujishughulisha nayo.
Jibu: Haidhuru akitafuta riziki. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Pupia yale yenye kukunufaisha.”
Akikusudia kutoa swadaqah, kufanya wema na kuwanufaisha watu ni mwenye kulipwa thawabu. Hivyo ndivo alivofanya as-Swiddiyq (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye alijitolea mali yake kwa ajili ya kuinusuru dini na kumuhami Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kumhudumia. Vivyo hivyo ´Umar alijitolea mali yake. Vilevile ´Abdur-Rahmaan bin ´Awf na Maswahabah wengine matajiri. Allaah aliwanufaisha waislamu kupitia wao.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22185/هل-يجوز-طلب-الدنيا-بنية-الاحسان-للناس
- Imechapishwa: 01/11/2022
Swali: Ibn-ul-Qayyim (Rahimahu Allaah) amesema kuwa mwenye kuitafuta dunia kwa lengo la kuwafanyia watu wema basi shaytwaan anakuwa mwenye kumpendezeshea nayo na hivyo anatumbukia katika kuipenda dunia na kujishughulisha nayo.
Jibu: Haidhuru akitafuta riziki. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Pupia yale yenye kukunufaisha.”
Akikusudia kutoa swadaqah, kufanya wema na kuwanufaisha watu ni mwenye kulipwa thawabu. Hivyo ndivo alivofanya as-Swiddiyq (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye alijitolea mali yake kwa ajili ya kuinusuru dini na kumuhami Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kumhudumia. Vivyo hivyo ´Umar alijitolea mali yake. Vilevile ´Abdur-Rahmaan bin ´Awf na Maswahabah wengine matajiri. Allaah aliwanufaisha waislamu kupitia wao.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22185/هل-يجوز-طلب-الدنيا-بنية-الاحسان-للناس
Imechapishwa: 01/11/2022
https://firqatunnajia.com/kuhangaika-na-dunia-kwa-ajili-ya-kuwafanyia-watu-wema/