Swali: `Allaamah Ibn-ul-Qayyim amesema:
“Kuna sampuli mbili za nyuchi:
1 – Uchi mkubwa
2 – Uchi mwepesi.
Akajumuisha mapaja miongoni mwa uchi mwepesi?
Jibu: Hapana shaka kuwa tupu ya nyuma na ya mbele ni katika nyuchi kubwa. Mapaja yanalinda ule uchi mkubwa. Maoni ya sawa ni kwamba ni uchi. Hadiyth tatu zinatiana nguvu; Hadiyth ya Muhammad bin Jahsh, Jarhad na Ibn ´Abbaas. Zinatiana nguvu na hivyo zinafuta yale yaliyomtokea Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Swali: Ambaye anavaa kaptula na nguo nyepesi?
Jibu: Haijuzu kufanya hivo. Ni lazima kufunika mapaja.
Swali: Mtoto wa kiume anatakiwa kufunika mapaja?
Jibu: Akishabaleghe. Salama na bora zaidi afunike mapaja akiwa ni mtoto wa miaka kumi na mfano wake. Isitoshe kunamuweka mbali zaidi na mtihani.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23721/حكم-ستر-الفخذين-للكبير-والصغير
- Imechapishwa: 14/04/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)