Swali: Kufunga Sha´baan inakuwa kamili au nusu yake?
Jibu: Afunge siku zake nyingi au yote. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akifunga siku zake nyingi au karibu yote isipokuwa siku chache.
Swali: Vipi maoni yanayosema kuwa mtu afunge siku kumi na tano za mwanzo kuanzia mwanzo wa Sha´baan?
Jibu: Hapana. Afunge siku zake nyingi au zote. Hii ndio Sunnah.
Swali: Je, inafaa kwake kuunganisha Sha´baan na Ramadhaan ikiwa ataanza Sha´baan kuanzia mwanzo wake au ale siku moja au siku mbili kati ya hizo mbili?
Jibu: Akila kati ya Sha´baan an Ramadhaan ndio bora zaidi. Vinginevyo inafaa kwake. Umm Salamah amesema:
“Alikuwa akiifunga [Sha´baan] yote.”
Katika upokezi mwingine kutoka kwa ´Aaishah:
“Alikuwa akiifunga [Sha´baan] yote.”
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22355/هل-السنة-صوم-شعبان-كله-او-بعضه
- Imechapishwa: 24/02/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)