Swali: Ikiwa mtu anaswali swalah nyingi zinazopendeza na baada ya kila Tasliym anabadilisha maeneo?
Jibu: Halina msingi.
Swali: Hadiyth ya al-Mughiyrah bin Shu´bah:
“Je, anashindwa yeyote katika nyinyi anapomaliza kuswali akasogea mbele au akarudi nyuma au akaenda kuliani au kushotoni?”
Jibu: Ni dhaifu.
Mwanafunzi: Viipi kitendo cha Ibn ´Umar?
Jibu: Hilo ni katika Ijtihaad yake.
Swali: Wako ambao wanajengea hoja kitendo hicho kwamba Siku ambayo ardhi itaelezea khabari zake ya kwamba ni kule mtu kuswali maeneo mbalimbali?
Jibu: Hapana, haina msingi. Aswali mahali pake. ´Ibaadah hazitokamani kwa khiyari au maoni ya mtu. ´Ibaadah ni kwa mujibu wa dalili.
Swali: Kwa hivyo bora mtu anapomaliza kuswali faradhi aswali mahali pake palepale?
Jibu: Mahali pake. Vinginevyo bora zaidi aenda kuswali nyumbani kwake.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23789/حكم-الانتقال-من-مكان-لاخر-في-صلاة-النافلة
- Imechapishwa: 01/05/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)