Swali: Je, inafaa kwa mume kumtembelea na kukaa wakati wa mchana kwa yule mke ambaye sio zamu yake?

Jibu: Kugawanya zamu ni usiku. Haina neno katika wakati wa mchana akamtembelea mmoja katika wakeze. Haina neno wakati wa mchana akawatembelea wakeze wengine na akaangalia ni nini wanachohitaji. Haina neno kufanya hivo. Mtume (Swalla Allaahu ´aayhi wa sallam) alikuwa akiwatembelea wakeze wakati wa mchana.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (38)
  • Imechapishwa: 23/06/2023