Swali: Hadiyth iliyo kabla yake inayozungumzia ambao watakuwa Motoni:
” Ataletwa mtu siku ya Qiyaamah na kuvugumizwa Motoni … ”?
Jibu: Hiyo ni Hadiyth ya Usaamah ya kwamba:
“Ataletwa mtu siku ya Qiyaamah na kuvugumizwa Motoni ambapo matumbo yake yatatoka nje. Atazunguka nayo kama punda anavozunguka kwenye kinu chake. Watu wa Motoni watakusanyika kwake na kusema: “Ee fulani! Una nini? Wewe si ulikuwa ukiamrisha mema na ukikataza maovu?” Aseme: “Nilikuwa nikikuamrisheni mema lakini mimi mwenyewe siyafanyi na nikikukatazeni maovu lakini lakini mimi mwenyewe nayafanya.”[1]
Anawaambia watu waswali lakini yeye haswali, anawakataza watu kuzini lakini yeye anazini na anawakataza watu kunywa pombe lakini yeye anakunywa pombe. Tunamuomba Allaah afya.
[1] Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb” (124).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/21538/جزاء-من-يامر-بالمعروف-ولا-ياتيه
- Imechapishwa: 20/08/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket