Swali: Katika Sunnah kumethibiti Takbiyr iliyofungamanishwa (Muqayyad)?
Jibu: Takbiyr iliyofungamanishwa kwa mujibu wa wanachuoni inakuwa baada ya zile swalah tano. Kuanzia siku ya ´Arafah mpaka ile siku ya mwisho ya Tashriyq. Mtu anatakiwa kuleta Takbiyr siku ya ´Arafah, siku ya ´Iyd na yale masiku matatu ya Tashriyq. Kwa mwenye kuhiji ni pindi atapohudhuria ile siku ya kuchinja atakaporusha mawe kwenye nguzo ya ´Aqabah. Hii ndio Takbiyr iliyofungamanishwa. Imechukuliwa katika maneno Yake (Ta´ala):
وَاذْكُرُوا اللَّـهَ فِي أَيَّامٍ مَّعْدُودَاتٍ
”Mtajeni Allaah katika siku za kuhesabika.”[1]
[1] 02:203
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (08) http://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=FullContent&audioid=191309#219638
- Imechapishwa: 20/01/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)