Ni yepi maoni yenye nguvu kuhusu ambaye anagusa msahafu ilihali yuko na hadathi?

Swali: Ni yepi maoni yenye nguvu kuhusu ambaye anagusa msahafu ilihali yuko na hadathi?

Jibu: Haijuzu kugusa msahafi ilihali mtu yuko na hadathi. Amesema (Ta´ala):

لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ

“Haigusi isipokuwa waliotwaharishwa kabisa.” (16:79)

Katika Hadiyth ya ´Amr bin Hazm ambaye amesimulia kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Haigusi Qur-aan isipokuwa yule mwenye twahara.”

Haya ndio maoni ya wale maimamu wane. Haifai kuigusa Qur-aan isipokuwa yule ambaye yuko na wudhuu´.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (08) http://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=FullContent&audioid=191309#219638
  • Imechapishwa: 20/01/2019