Swali: Nikiingia ndani ya swalah punde kidogo kabla ya Rukuu´ ni jambo limesuniwa kusoma al-Faatihah au nisome du´aa ya kufungulia swalah? Imamu akirukuu kabla sijamaliza kusoma al-Faatihah nifanye kitu gani?
Jibu: Kusoma du´aa ya kufungulia swalah imependekezwa na kusoma al-Faatihah ni jambo la faradhi kwa maamuma kwa mujibu wa maoni sahihi ya wanazuoni. Ukikhofia kwamba utakosa al-Faatihah basi anza nayo. Pindi imamu ataporukuu kabla hujaikamilisha basi rukuu pamoja naye na inakundondokea sehemu yake nyingine iliobaki. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika si venginevyo imamu amewekwa ili afuatwe. Hivyo basi msitofautiane naye. Akisema “Allaahu Akbar” nanyi semeni “Allaahu Akbar” na akirukuu nanyi rukuuni.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
[1] al-Bukhaariy (680) na Muslim (625).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/243)
- Imechapishwa: 28/10/2021
Swali: Nikiingia ndani ya swalah punde kidogo kabla ya Rukuu´ ni jambo limesuniwa kusoma al-Faatihah au nisome du´aa ya kufungulia swalah? Imamu akirukuu kabla sijamaliza kusoma al-Faatihah nifanye kitu gani?
Jibu: Kusoma du´aa ya kufungulia swalah imependekezwa na kusoma al-Faatihah ni jambo la faradhi kwa maamuma kwa mujibu wa maoni sahihi ya wanazuoni. Ukikhofia kwamba utakosa al-Faatihah basi anza nayo. Pindi imamu ataporukuu kabla hujaikamilisha basi rukuu pamoja naye na inakundondokea sehemu yake nyingine iliobaki. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika si venginevyo imamu amewekwa ili afuatwe. Hivyo basi msitofautiane naye. Akisema “Allaahu Akbar” nanyi semeni “Allaahu Akbar” na akirukuu nanyi rukuuni.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
[1] al-Bukhaariy (680) na Muslim (625).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/243)
Imechapishwa: 28/10/2021
https://firqatunnajia.com/katika-hali-hii-tanguliza-al-faatihah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)