Swali: Mtu akiwa ni msafiri na akasikia adhaana aswali na mkusanyiko?
Jibu: Ni sawa ikiwa ni wepesi. Vinginevyo yuko na safari ikiwa anachelea anaotangamana nao au kitu kitachompita. Katika hali hiyo aendelee na safari na aswali njiani.
Swali: Akikosa swalah ya mkusanyiko kisha akarudi nyumbani – je, aiswali kwa kufupisha?
Jibu: Aswali kwa kufupisha Rak´ah mbili. Hilo linahusu Dhuhr, ´Aswr na ´Ishaa. Akiswali na wengine basi aiswali Rak´ah nne.
Swali: Je, analazimika kuswali na mkusanyiko asiposikia adhaana?
Jibu: Analazimika akiwa yuko peke yake. Lakini akiwa na wengine ni mwenye khiyari; wakitaka wataswali wenyewe hali ya kufupisha na wakitaka wataswali na mkusanyiko na wengine na hivyo watakamilisha Rak´ah nne.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22551/هل-تجب-الجماعة-للمسافر-لو-سمع-النداء
- Imechapishwa: 07/07/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)