Je, “Rifqan Ahl-as-Sunnah bi Ahl-is-Sunnah” ni utetezi kwa al-Ma´ribiy?

Swali: Je, ni kweli zile tetesi zinazoenezwa kwamba Shaykh ´Abdul-Muhsin al-´Abbaad aliandika kitabu hiki (Rifqan Ahl-as-Sunnah bi Ahl-is-Sunnah) kwa ajili ya kumtetea Abul-Hasaan [al-Ma´ribiy]?

Jibu: Kamwe, kamwe, kamwe, kamwe. Shaykh wetu ´Abdul-Muhsin aliulizwa swali hilo msikitini ambapo akasema kuwa amekiandika kwa ajili ya ndugu zetu Ahl-us-Sunnah, Salafiyyuun, na si wengine. Akasema kuwa hakuwakusudia al-Ikhwaan al-Muslimuun, Jamaa´at-ut-Tabliygh, huyu wala yule. Kitabu ”Rifqan Ahl-as-Sunnah bi Ahl-is-Sunnah” amewakusudia kuwanasihi ndugu zake Ahl-us-Sunnah. Hivo ndivo alivosema.

  • Mhusika: Shaykh Swaalih bin Sa´d as-Suhaymiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://youtu.be/K7SBpXfA4Qw
  • Imechapishwa: 05/11/2022