Swali: Kumekuja maswali mengi kuhusu Jamaa´at-ut-Tabliygh.

Jibu: Jamaa´at-ut-Tabliygh ni jambo linalojulikana ya kwamba ni Suufiyyah. Na wala hatuwanasihi kutoka pamoja nao, kwa kuwa hawalinganii katika Tawhiyd na wala hawaamrisha mema na wala hawakatazi munkari. Wanaamrisha watu: “fanyeni khuruuj! Fanyeni khuruuj! Fanyeni khuruuj! Siku arobaini, siku tatu, mara mbili kwa kila wiki, na kila mwezi mara tatu. Haya yote hayana dalili. Wanaita kufanya hivi ya kwamba ni katika “Sabiyli Allaah” (njia ya Allaah). Wanatilia umuhimu Adhkaar tu kuwanasihi baadhi ya wajinga na kuwalingania. Hawana elimu. Hawana elimu.

Tunawanasihi vijana wasifanye khuruuj na badala yake watafute elimu na wasifanye khuruuj. Na akitaka mtu kulingania baada ya kupata elimu, alinganie katika dini ya Allaah. Ama kutoka ilihali ni mjinga asiyejijua na wala hafahamu kitu, hapana. Baadhi ya wazee wakubwa wanawaacha waongee, wazee wakubwa wasiofahamu lolote kabisa wanawaacha waongee msikitini na watoe nasaha. Na mara wanaachia vijana wasiofahamu lolote. Isitoshe hawalinganii katika Tawhiyd na wala hawakatazi munkari. [Wanamwambia] “Lingania katika kadhaa na kadhaa na wala usimwongelee mtu yeyote.”

Makusudio yetu, sisi tunawanasihi jitahidini kutafuta elimu, jifunzeni na muwe na ufahamu katika dini, kisha baada ya hapo alinganie katika dini ya Allaah.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.ajurry.com/vb/showthread.php?t=35571
  • Imechapishwa: 03/09/2020