Swali: Kuhusiana na kisa ambacho kinasimuliwa na maimamu wa Da´wah ambapo wanasema namna baadhi ya Maswahabah walipata mwili wa Nabii Daaniyaal kisha wakalificha kaburi lake ili lisifanywe kuwa ni mahali pa kuswalia. Je, kisa hiki ni sahihi?
al-Albaaniy: Nini unachokusudia watu wa Da´wah?
Muulizaji: Mjukuu wa Shaykh Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab.
al-Albaaniy: Istilahi hiyo hii leo inatumiwa kwa Jamaa´at-ut-Tabliygh.
Muulizaji: Hapana, sikuwakusudii wao.
al-Albaaniy: Najua hukuwakusudia wao, lakini mtu anaweza kufahamu hivo. Kwa ajili hiyo ndio maana nikashangazwa kutokana na nilivofahamu. Kwa sababu watu hawa hawatilii umuhimu mambo haya kabisa – mambo kuhusu Tawhiyd. Kwa hali yoyote, kisa ni sahihi na kina msingi uliyothibiti.
- Muhusika: Imâm Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Silsilat-ul-Hudaa wan-Nuur (304)
- Imechapishwa: 14/05/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)