Swali: Tunafanya katika katika dula la kuuza nguo. Katika mwezi wa Ramadhaan kumi la mwisho hatuwezi kukaa I´tikaaf wakati wa mchana kutokana na mazingira ya kazi. Je, ni sahihi kukaa I´tikaaf wakati wa usiku peke yake na mchana tukafanya kazi dukani?
Jibu: Inafaa kufanya I´tikaaf ijapo kitambo fulani cha muda ndani ya msikiti ambao kunaswaliwa swalah ya mkusanyiko. Ni sahihi kufanya I´tikaaf kama mtu hakufunga kwa mujibu wa maoni sahihi zaidi ya wanazuoni. ´Abdullaah bin ´Umar amepokea kupitia kwa baba yake (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ya kwamba alisema:
“Ee Mtume wa Allaah! Hakika mimi kipindi kabla ya Uislamu niliweka nadhiri ya kukaa I´tikaaf usiku mmoja katika msikiti Mtakatifu.” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Tekeleza nadhiri yako!” Akafanya I´tikaaf usiku mmoja.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim katika ”as-Swahiyh” zao na tamko hili ni la al-Bukhaariy (02/260). Kama swawm ingelikuwa ni sharti ya kusihi kwa I´tikaaf, basi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) asingemkubalia kufanya I´tikaaf wakati wa usiku peke yake. Kwa hivyo inafaa kwenu kuweka kikomo cha nia ya kukaa I´tikaaf wakati wa usiku peke yake pasi na mchana kutokana na mliyotaja. Mnapata thawabu kwa kiasi chenu – Allaah akitaka.
- Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (09/321) nr. (18979)
- Imechapishwa: 23/04/2022
Swali: Tunafanya katika katika dula la kuuza nguo. Katika mwezi wa Ramadhaan kumi la mwisho hatuwezi kukaa I´tikaaf wakati wa mchana kutokana na mazingira ya kazi. Je, ni sahihi kukaa I´tikaaf wakati wa usiku peke yake na mchana tukafanya kazi dukani?
Jibu: Inafaa kufanya I´tikaaf ijapo kitambo fulani cha muda ndani ya msikiti ambao kunaswaliwa swalah ya mkusanyiko. Ni sahihi kufanya I´tikaaf kama mtu hakufunga kwa mujibu wa maoni sahihi zaidi ya wanazuoni. ´Abdullaah bin ´Umar amepokea kupitia kwa baba yake (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ya kwamba alisema:
“Ee Mtume wa Allaah! Hakika mimi kipindi kabla ya Uislamu niliweka nadhiri ya kukaa I´tikaaf usiku mmoja katika msikiti Mtakatifu.” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Tekeleza nadhiri yako!” Akafanya I´tikaaf usiku mmoja.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim katika ”as-Swahiyh” zao na tamko hili ni la al-Bukhaariy (02/260). Kama swawm ingelikuwa ni sharti ya kusihi kwa I´tikaaf, basi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) asingemkubalia kufanya I´tikaaf wakati wa usiku peke yake. Kwa hivyo inafaa kwenu kuweka kikomo cha nia ya kukaa I´tikaaf wakati wa usiku peke yake pasi na mchana kutokana na mliyotaja. Mnapata thawabu kwa kiasi chenu – Allaah akitaka.
Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (09/321) nr. (18979)
Imechapishwa: 23/04/2022
https://firqatunnajia.com/itikaaf-usiku-peke-yake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
