ISIS si kabisa mapando ya Salafiyyah

Makundi yote ya sasa yanayojishughulisha na Da´wah yako kwenye upotevu na matamanio. Kutokana na sababu hiyo Waislamu, wa kawaida na wasomi, wajitenge nayo mbali. Ikiwa hawakupokea ubainisho huu, basi kwa hakika ni wenye kumuasi Allaah, Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na mtawala wa Waislamu. Hii ni dhambi kubwa.

Ninasema haya hata kama wapinzani wa makundi kati ya Jamaa´at-ut-Tabliygh, al-Ikhwaan al-Muslimuun, watoto wa mapote yao na wale wanaochukua kutoka kwao watachukulia hilo kwa ubaya.

Kundi liloongoka ambalo limeshikamana na haki na Sunnah ni Salafiyyah. Adui mmoja wa Allaah amesema uongo pindi aliposema kuwa ISIS ni mapando ya Salafiyyah.

  • Mhusika: Shaykh ´Ubayd bin ´Abdillaah al-Jaabiriy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=146597
  • Imechapishwa: 19/04/2015